У нас вы можете посмотреть бесплатно PIGO KWA DRC, WAZALENDO WASALITI WAJIUNGA M23, MAREKANI YAOMBA KUINGILIA KATI или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Goma. Takriban vikundi vitatu vya wapiganaji wa kundi la Wazalendo wanaoliunga mkono Jeshi la Serikali Jamhuri Kidemokrasia ya Congo (DRC) la FARDC huko Kivu Kaskazini wameasi na kujiunga na muungano wa makundi ya waasi wa Alliance Fleuve Congo (AFC/M23). Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini DRC, taarifa iliyosainiwa na kiongozi wa Wazalendo, Shukuru Bulenda, vikundi hivyo vilivyoasi ni pamoja na Mai-Mai Kabidon (FPP-AP), sehemu za Mai-Mai Kifuafua na kikundi cha Nduma Defense of Congo-Renovated (NDC-R/M). Vikundi hivyo, vinadaiwa kujiunga na AFC/M23, juzi Machi 9,2025. Kituo cha habari cha Kivu Morning Post kiliripoti jana kuwa wapiganaji wa muungano huo mpya walikuwa wakielekea kaskazini kutoka ngome zao za Kivu Kaskazini na Kusini kuelekea kijiji cha Kasugho, takriban maili 28 magharibi mwa wilaya ya Lubero kwa lengo la kupambana na FARDC. M23 imekuwa ikijaribu kuzunguka ngome za FARDC katika mji wa Lubero tangu mwishoni mwa Februari bila mafanikio. M23 iliuteka Mji wa Kasugho Machi 2, mwaka huu, kabla ya kuondoka Machi 7 na kuelekea Bunyatenge, eneo lenye machimbo ya dhahabu lililo umbali wa saa 6 kutoka Kasugho nchini humo. Vyombo vya habari vya DRC vimesema uasi wa wapiganaji wa FPP-AP kujiunga na M23 ni pigo kubwa kwa jeshi la FARDC katika mapambano ya kuidhibiti M23. Pia vimeielezea FPP-AP kama moja ya vikundi vyenye muundo mzuri na ushawishi mkubwa katika Jimbo la Kivu Kaskazini ambavyo vilikuwa vimepeleka mamia ya wapiganaji kwenye vijiji kadhaa katika wilaya ya Lubero ili kuwazuia M23 kusonga mbele kuelekea Lubero, Butembo na Mji wa Beni. Kituo cha habari cha DRC, Actualite.cd, kilisema kwamba FPP-AP ina ushawishi mkubwa katika wilaya ya Kaskazini magharibi ya Lubero, hasa katika mji wa machimbo ya dhahabu wa Maguredjipa, ulio maili 73 Kaskazini Magharibi mwa mji wa Lubero na unapakana na jimbo jirani la Tshopo. Kituo hicho, kilimnukuu mtafiti wa ndani aliyesema kuwa kuingizwa kwa FPP-AP katika muundo wa muungano wa M23 kutairuhusu M23 kusonga mbele bila kuzuiliwa kutoka Kasugho hadi Manguredjipa kupitia Bunyatenge.