У нас вы можете посмотреть бесплатно ADAIWA KUMPIGA RISASI DEREVA ALIYEKUWA AMEPAKI GARI VIBAYA NA KUSABABISHA KIFO CHA MKEWE ARUSHA. или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Mwanaume anayefahamika kwa jina la John Peter (45) mkazi wa eneo la Manyire wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, anadaiwa amemjeruhi dereva wa Scania kwa risasi baada ya gari lake aina ya Noah kugonga kwa nyuma Scania hiyo na kusababisha mke wake aitwae Lucy John (40) kufariki dunia papo hapo katika eneo la Nganana wilayani humo. Mmoja wa mashuhuda katika tukio hilo akizungumza na GADI TV amesema dereva huyo alipigwa risasi mbele yake na baada ya hapo ndugu Peter alianza kuwakimbiza waliokuwa wamefika kushuhudia tukio hilo huku akisikika akidai kuwa watu hao hawawezi kutoa msaada wakuweza kurejesha uhai wa mkewe katika usiku wa tukio hilo, February 11, 2025. Kwa upande wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha Justine Masejo, imesema baada ya ndugu John kugonga Scania hiyo kwa nyuma, John alianza kumshambulia dereva huyo anayejulikana kwa jina la Jafari Shirima (62) kwa kutumia kitu chenye ncha kali na kumsababishia majeraha mbalimbali katika mwili wake. Katika hatua nyingine, GADI TV imefanya jitihada za kumtafuta Jafari na tumefanikiwa kumpata akiwa anaendelea kupatiwa matibabu katika moja ya Hosptali mkoani humo, na ametueleza kuwa alipigwa risasi ya tumbo, mkononi na mguuni kwa madai kuwa aliegesha gari hilo barabarani bila tahadhari na kusababisha ajali hiyo. Aidha, Shirima amesema kwasasa anaendelea vizuri baada ya matibabu, pia anawashukuru madaktari wote waliojitahidi kuokoa maisha yake. #breakingnews #trendingvideo #lifestyle #live #livestream #trendingshorts #trending GADI TV ndiyo Channel pekee inayokuwezesha kupata Habari za Kisiasa,Michezo, Kijamii, na Burudani kutoka Ndani na Nje ya Tanzania. Kwa huduma ya Matangazo au Habari pamoja na maoni na ushauri usisite kuwasiliana nasi kupitia namba za simu +255 769 780 063 au e-mail: [email protected] Don't forget to SUBSCRIBE, LIKE, COMMENT and SHARE!!! # GADI TV Thanks.