У нас вы можете посмотреть бесплатно Je kuna Laana na Maagano ya Familia na ukoo kwa waliomuamini YESU KRISTO !? Mwl.Bryan или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Katika video hii nimeeleza kuhusu JE LAANA ZA VIZAZI NA MAAGANO ya KOO HUMFUATA ALIYE KATIKA KRISTO. Dhambi ya urithi. • DHAMBI: Je DHAMBI YA URITHI INAENDELEA ktk... Wapendwa kwanza kabisa Tujue maana ya laana na agano kabla hatuja enda Mbali. Laana ni Hukumu itolewaje Baada ya kukosea kitu Fulani au Kuvunja Sheria Fulani. Hasa kwenye Mfumo mkuu huaribu mtiririko mzima. MAAGANO ya kifamilia muundo wa familia unarejelea njia zinazorudiwa za wanafamilia kuingiliana, kuishi, au uzoefu wa maisha, zinazojumuisha mienendo ya uhusiano na sifa za kizazi zinazorudiwa, zote chanya (mawasiliano ya kiafya) na hasi (uraibu,umasikini, Magonjwa nk). Mifumo hii hufunzwa na kupitishwa, kuathiri maisha ya mtu binafsi. Basi sawa kabisa Mtu asiye katika Kristo kusema kuna MAAGANO, Laana inayomfuatilia,.lakini kwa aliye KATIKA KRISTO hicho kitu Sio sawa na nimakosa Makubwa sana na unabadilisha Maana kabisa ya Yesu Kuja KWETU. Tena haiwezekani kuwa katika MAAGANO ya ukoo arafu ukiwa katika Kristo. Wagalatia 3:13 Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; Ikiwa Kwa Adamu (Mtu mmoja ) Dhambi ilingia na kwa YESU Dhami na laana Zote zilifutwa na MAAGANO. Ya mauti na mambo Mengine Mengi. ( Warumi 5:12, 17-18 12 Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi 18 Basi tena, kama kwa kosa moja watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima. MIFUMO MIWILI. Basi kama ukibadilisha Mfumo Hapo pia mzunguko hauwezi kuwa ule ule wa mwanzo hauwezi kuchuma mapera kwenye Muembe Wala zabibu kwenye Mgomba. YEREMIA 31:29-34… Yeremia 31:29-33 29 Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi. 30 Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi. 31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda. 32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana. 33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. • DHAMBI: Je DHAMBI YA URITHI INAENDELEA ktk... Upya . Ezekiel anazungumzia pia jambo hili juu ya Agano Jipya na Mfumo mpyaa wa kuto kuchukua Uovu wa Baba yake. Ezekieli 18:2, 4-5 2 Je! Maana yake ni nini hata mkatumia mithali hii katika Israeli, mkisema, Baba wamekula zabibu mbichi, nao watoto wakatiwa ganzi la meno? 4 Tazama, roho zote ni mali yangu; kama vile roho ya baba ni mali yangu, ndivyo ilivyo roho ya mwana mali yangu; roho ile itendayo dhambi itakufa. 5 Bali kama mtu ni mwenye haki, na kuyatenda yaliyo halali na haki; KUZALIWA MARA YA PILI. Basi Mtu anapo zaliwa mara ya Pili yaani kufa arafu ukazaliwa upya Basi Hapo hakuna Tena laana maana tunakuwa wana. 1 John 3:1-2. 1 Yohana 3:1-2 1 Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. 2 Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. So tunakuwa tumezaliwa katika KRISTO na Damu yetu na DNA inasoma YESU. Hapo Anza kujiuliza Maswali kama umemuamini kristo unayosema ni MAAGANO ya ukoo na Familia je Niya kwa MUNGU. Soma Galatia 5:22-24. Neno kanisa limetokana na Neno Ekklesia maana yake ( ek out (kutoka) kaleo ( kuitwa) maana yake ni Wale walio itwa kutoka kwenye kundi Fulani na hapa wokovu nikuwa tunaitwa kutoka katika Ule mnyororo wa Asili na kuumbwa upya. Muito wa kwanza ukitoka kwa Abraham Mwanzo 12.. kutoka kwa familia yake na Baba zake. Hivyo hauitaji Kupingana na MAAGANO ya Familia Yako ila nikitoka kati Yako nako ni kwakumuamini YESU. Mfano wa Ruthu alikuwa ni (mmoabi ) ambayo Hapo wa Moabu kwenye Kumbukumbu la Torati 23:3 Anasema Mungu “Mwamoni wala Mmoabi wasiingie katika mkutano wa Bwana; wala hata kizazi cha kumi mtu wao asiingie katika mkutano wa Bwana milele;”. Hivyo ilikuwa ni laana kwake. Ruthu Tunaona anamwambia Naomi ma mkwe kuwa Ruthu 1:16-17 16 Naye Ruthuu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu; Maneno yale yale MUNGU alimwambia Na Abraham kwenye Mwanzo 17. Nitakuwa MUNGU wako. Ruthu anaingia Kwenye Baraka Kwa kuolewa na Boazi na Wafalme wote wanatoka kwake Haya na Ile laana ya Wamoabi haimfuati Tena. #yesu #mungu #2026