У нас вы можете посмотреть бесплатно MAGONJWA YA NGONO: Sababu, Dalili, Matibabu или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Katika video hii inazungumza kuhusu sababu, dalili, matibabu, namna ya kuzuia, matarajio baada ya matibabu ya MAGONJWA YA NGONO, endelea angalia mpaka mwisho kujifunza. Magonjwa ya ngono ni magonjwa yanayoambukiza kwa njia ya tendo la kujamiiana na mtu aliyeambukizwa bila kutumia kondomu. Tunaposema kujamiiana tunamaanisha kuingiza uume- ukeni au uume kwenye sehemu ya haja kubwa au kunyonyana sehemu za siri. Magonjwa haya yanaweza kuwapata watu wa rika na jinsi zote hususani wale wenye umri wa kuzaa (kati ya miaka 15-49) Vijana wenye umri kati ya miaka 10 hadi 24 wanawakilisha moja ya tatu (1/3) ya idadi ya watu wote wa nchi za Afrika ikiwemo Tanzania. Kundi hili liko katika hatari zaidi ya maabukizi ya magonjwa ya ngono kwa kuwa wanapobalehe wanapata hisia za kupenda na pia hamu ya kufanya tendo la kujamiiana inakuwa kubwa kwa sababu ya homoni za mwili. Kwa hiyo, kama hawana uelewa mzuri kuhusu miili yao, wanaweza kujiingiza katika tabia hatarishi za kujamiiana bila kondomu au kujamiiana na wapenzi wengi. Aina za magonjwa ya ngono Kuna aina mbalimbali za magonjwa ya ngono ambayo yamegawanywa katika makundi kutokana na dalili zake: • Magonjwa yenye dalili za kutokwa na usaha au majimaji sehemu za siri (ukeni au uumeni) ambayo ni Kisonono, Trikomonas na Kandida • Magonjwa yenye dalili za kutokwa na vidonda ambayo ni Kaswende, Pangusa na Malengelenge sehemu za siri • Magonjwa yenye dalili za kutokwa na uvimbe ambayo ni Mitoki, Pangusa na Malengelenge sehemu za siri Mtu anaweza kuwa na zaidi ya ugonjwa mmoja wa ngono kwa wakati mmoja. Kuna watu ambao wanaweza kupata ugonjwa wa ngono, lakini wasipate dalili zozote. kwa mfano - Asilimia 10-15 ya wanaume na asilimia 60-70 ya wanawake wenye kisonono hawaoneshi dalili yoyote. Kwa hiyo, kama una mpenzi mpya, kabla ya kujamiiana – unashauriwa kwenda kituo cha afya kupata vipimo vya magonjwa ya ngono. Dalili za Magonjwa ya ngono Kwa vijana wa kike, magonjwa ya ngono yanaweza kusababisha ukapata • Maumivu chini ya kitovu • Kutokwa na usaha au majimaji yenye harufu mbaya sehemu za siri • Kuwashwa sehemu za siri • Vidonda na upele sehemu za siri, mdomoni na sehemu nyingine za mwili • Maumivu wakati wa kujamiiana • Kuvimba mtoki • Kuota sundosundo sehemu za siri • Kukojoa mara kwa mara kunakoambatana na ,muwasho au maumivu Kwa kijana wa kiume wanapata: • Maumivu makali sehemu za siri wakati wa kukojoa • Kutokwa na usaha sehemu za siri • Vidonda sehemu za siri • Vidonda sehemu za mdomoni • Kuvimba mtoki • Kupata melengelenge • Kuota sundosundo sehemu za siri Tabia zinazoongeza hatari ya kuambukizwa magonjwa ya ngono Baadhi ya tabia zinaongeza uwezekano wa kupata magonjwa ya ngono: • Kujamiiana bila kondomu • Kujihusisha na ukahaba • Kujamiiana na wapenzi wengi • Kunyonyana sehemu za siri • Kunyonyana ndimi (kula denda) –Kisonono, Kaswende na virusi vya UKIMWI • Woga wa vijana wa kike kuwashawishi vijana wa kiume kutumia kondomu wakati wa kujamiana kwa sababu ya mfumo dume. • Tamaa ya kupata pesa pamoja na vitu vya thamani kama simu za mikononi, magari kutoka kwa watu mbalimbali • Kuhusika na vitendo vya ubakaji • Utumiaji wa madawa ya kulevya au pombe ambayo husababisha kijana kukosa ufahamu na hivyo kufanya ngono isiyo salama. • Ushoga Athari za magonjwa ya ngono Magonjwa ya ngono yasipotibiwa mapema na kwa usahihi yanaweza kuleta athari: Kwa kijana wa kike • Kuziba kwa mirija ya uzazi ambako kunasababisha aidha mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi au ugumba • Maambukizi katika mfuko wa uzazi • Kupata magonjwa katika viungo muhimu mwilini • Magonjwa ya moyo na mishipa ya damu • Kansa ya kizazi • Mabadiliko ya hedhi • UKIMWI Kwa kijana wa kiume • Maambukizi katika kokwa za mbegu za uzazi • Kuziba mirija inayopitisha mbegu za uzazi na kuleta utasa • Kupata matatizo ya kukojoa kwa sababu ya kuziba njia ya mkojo • Kupata magonjwa katika viungo muhimu mwilini kama ubongo, moyo, na figo • Kansa ya uume • Kupungua nguvu za kiume • UKIMWI Athari zote hizi zinaweza kuepukika iwapo magonjwa ya ngono yatatibiwa mapema na kwa Emmanuel Mniko #mniko #wikielimu @wikielimu