У нас вы можете посмотреть бесплатно 🛑 LIVE MAJIZO AWAOMBEA MSAMAHA WASANII KWA WANANCHI, WATAKUFA NA NJAA TUWAONEE HURUMA TUSIMAME NAO или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
MAJIZO AWAOMBEA MSAMAHA WASANII KWA WANANCHI Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya EML Afracis Anthony maarufu (Majizo) ametoa pole kwa Watanzania wote waliofikwa na madhara baada ya Uchanguzi Mkuu October 29. Akizungumza kupitia mitandao yake kijamii amesema wasanii wa muziki wametumika muda mrefu kwenye siasa toka muda mrefu kila mmoja amekuwa anaitikadi naye. Majizo Amesisitiza kuwa wasanii wasiukumiwe kutumika Kwenye siasa bali Kila mmoja anatafuta riziki kwenye sekta mbalimbali ikiwemo siasa. "Natoa pole kwa yote yaliyotukuta baada ya Uchaguzi wa Oktoba 29, kubwa zaidi wale waliopata misiba. Natambua maumivu yenu, Mungu mwenyewe awe mfariji kwenu. Pole kwetu sote. Nimejiridhisha kwamba huu ni wakati sahihi kuja kwenu kuzungumza, lengo langu mahsusi ikiwa Sekta ya muziki na hasara tunayotengeneza kwa Watanzania wanyonge" Ni kweli wasanii wwanaathirika Lakini athari kubwa zaidi, ipo kwa kundi kubwa linalotegemea hizo kazi za sanaa. Dancers wana kosa gani? Wapiga vyombo, Make up artists, Wauza Nguo, na wengine wengi? Familia zao vipi? Moja vilio ambavyo tunalia wote, ni kilio cha ukosefu wa ajira, hivyo tusizipige teke hizi ajira kwenye kiwanda cha muziki kwa sababu kuna watu wachache wametukasirisha. Ninaposema nimewahi kumchangia Sugu pesa sio kwamba alikuwa na shida binafsi, Sugu ni taita anayo pesa ya kutosha. Pesa ninayoongelea hapa ni ya kusaidia harakati za Muziki kupitia Bongo Flavour Honors. Na namtaja Sugu kama mfano wa wengi ambao wametumia maisha yao yote kuukuza muziki wetu, hata wao walipochagua vyama hawakutengwa na watu wa vyama vingine. Sugu hakuwahi kusema wanachama wa CCM wasije kwenye show zake au wasisikilize muziki wake. Nawaita kina Sugu na watu wengine, tusiruhusu muziki uanguke kwa sababu ya tofauti zetu za kiitikadi. Msamaha ninaoomba ni kwa sababu nafahamu kuna mahali wadogo zangu hawa walipitiliza na sio kwa sababu walifanya kampeni (ile ni haki yao na uamuzi wao). Najua kuna maneno yalikukera, sio katika level ya siasa, bali katika level ya utu. NAOMBA MSAMAHA. Huu muziki ni wenu. Mkiumiza tasnia, mnaumiza maelfu ya ajira. Kina Shilole hao wanaweza kutufikia sisi siku moja moja ukamtoa, vipi kuhusu wale wafanyakazi wake? Diamond na wengine, Mungu amewajaalia riziki, lakini unawaza kuhusu ajira zinazopotea kwa sababu ya hasira yako kwake? Naomba Radhi, na ikiwapendeza naomba muendelee kuupa nguvu Muziki wenu. Haya wananchi Mmepokea Ombi la MAJIZO kuwasamehe wasanii au waoambane na Hali zao? #Majizo #Bongoflava #SiasaZaTanzania