У нас вы можете посмотреть бесплатно Ukweli Kuhusu Ufugaji wa Kuku Chotara Tanzania - KUROILER или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
UFUGAJI WA KUKU CHOTARA Ufugaji wa kuku Chotara ni Ufugaji wa kibiashara na unapotaka kuanza biashara yeyote ni muhimu ukawa na mpango thabiti wa namna gani utaiendea biashara hiyo ili iweze kukuwa na kukupa mafanikio makubwa na unayoyahitaji. Jifunze Zaidi: • Ufugaji wa Kuku Chotara Biashara Biashara ya ufugaji wa kuku chotara imegawanyika katika makundi tofautitofauti, makundi hayo ni kama yafatayo:- 1. Uzalishaji wa mayai au vifaranga au vyote kwa pamoja 2. Uzalishaji wa vifaranga wa wiki 4-5 3. Uzalishaji wa kuku chotara kwaajili ya nyama Kabla haujaanza ufugaji wa kuku chotara yakupasa uwe umechagua ni aina gani ya bidhaa unataka kuingiza sokoni. Soko kubwa la kuku chotara ni wafugaji ambao wanataka kuingia kwenye biashara hiyo, kwahiyo yakupasa mhamasishaji na uwe na ushiwishi kwa wengine ili kujitanulia soko. Lakini zipo hatua ambazo inakubidi uzifahamu na uzipitie ili uweze kufuga kuku chotara kwa mafanikio. Hatua hizo ni kama zifatazo:- 1. Unahitaji Kuzalisha Bidhaa ya aina gani ._ Kama nilivyotangulia kusema hapo awali kuwa ufugaji wa kuku chotara umegawanyika katika makundi tofautitofauti, unapo hitaji kuanza ufugaji wa kuku chotara unatakiwa kuchagua kundi moja na ukawekeza nguvu ya kutosha ili kuongeza thamani ya utakachozalisha. Kundi la 1. Uzalishaji wa mayai au vifaranga au vyote kwa pamoja. Katika kundi hili, mfugaji wa kuku chotara anatakiwa kuwa na kuku wazazi watakao kuwa wanazalisha mayai kwaajili ya biashara, au kutotoleshe vifaranga kwaajili ya biashara au kufanya vyote kwa pamoja, kuzalisha mayai na kuuza vifaranga. Uwekezaji kwenye kundi la kwanza unahitaji mtaji mkubwa kidogo hivyo unapaswa kujiandaa vizuri ili uweze kuwahudumia na kuwapa mazingira mazuri kuku wazazi. Kundi la 2. Uzalishaji wa vifaranga wa wiki 4-5 Katika kundi hili mfugaji wa kuku chotara anatakiwa kuwa na banda la kulelea vifaranga mpaka watakapo fikisha wiki 4 -5. Sio lazima kwa mfugaji kwenye kundi hili kuwa na kuku wazazi, unachotakiwa kufanya ni kutafuta wazalishaji wa vifaranga bora vya kuku chotara ambao watakuwa wakikuhudumia vifaranga kwaajili ya biashara yako. Kitu muhimu cha kuzingatia ni kuhakikisha, vifaranga wanapata chakula bora na chanjo zote za muhimu kwa wakati. Vilevile muwekezaji kwenye kundi la kwanza anaweza akafanya biashara hii kama atakuwa na eneo la kutosha kwa sababu wafugaji wengi wanaoanza wanaogopa kulea vifaranga wa siku moja. Kundi la 3. Uzalishaji wa kuku wa nyama Katika kundi hili mfugaji wa kuku chotara anatakiwa kuwalea vifaranga mpaka watakapofiksha wiki 10-12 ambapo watakuwa tayari wamepevuka kwaajili ya nyama. Sio lazima kwa muwekezaji katika kundi hili kuwa na kuku wazazi, unachotakiwa kufanya ni kutafuta wazalishaji bora wa vifaranga vya kuku chotara atakaye kuwa anakuhudumia vifaranga kwaajili ya biashara yako. Kitu cha kuzingatia kwenye uwekezaji huu ni kuwalisha chakula bora na ambacho hakina gharama kubwa ili uweze kupata faida. 2. Kutafuta elimu ya ufugaji wa kuku chotara._ Elimu ya ufugaji wa kuku chotara ni muhimu sana na itakupa mwanga wa utakachenda kukifanya. Elimu hiyo ihusishe vitu vifatavyo;- I. Ujenzi wa Banda la kuku chotara Katika vitu ambavyo mfugaji wa kuku chotara unanatakiwa kuvizingatia ni ujenzi wa banda la kuku kwa sababu hawa kuku chotara wanaathiriwa sana na hali ya hewa inayosababishwa na mazingira ukilinganisha na kuku wa kienyeji. Wafugaji waliojenga mabanda bora wamafanikiwa kupunguza changamoto za magojwa kwa kiasi kikubwa. II. Utaratibu wa kuwapa chanjo vifaranga Hili halina mjadala, ili kuwakinga kuku wako dhidi ya magonjwa yasiyokuwa na tiba na ambayo husababisha vifo kwa asilimia kubwa ni kuwa na elimu ya kuwapa chanjo kwa wakati. III. Udhibiti wa Magonjwa mbalimbali yanayosababisha vifo kwa kuku, magonjwa haya ni magonjwa ya miripuko kama typhoid, kipindupindu, coccidiosis, Coryza n.k IV. Jinsi ya kuwalisha kuku kwenye umri tofauti ili kuhakikisha wanakuwa vizuri na wanataga mayai mengi. V. Mbinu za kupunguza gharama za ulishaji wa chakula, mfano kuwalisha hydroponics na Azolla n.k. 3. Fahamu bajeti ya uendeshaji wa mradi._ Fanya hesabu ya kila kitu kinachohitajika ili kufahamu bajeti ya uendesgaji wa mradi, kuanzia vifaranga wanaingia bandani mpaka kufikia uzalishaji. Hesabu hiyo ihusishe vitu vifatavyo:- I. Gharama ya ujenzi wa banda II. Vifaa muhimu bandani Vyombo vya chakula na maji kwenye umri tofauti, vyanzo vya joto (jiko au balb), bruda, thermometer, mkaa, maranda na magazeti III. Chakula kwa rika tofauti Gharama ya chakula watakachokula mpaka waanze uzalishaji IV. Chanjo na antibiotiki Gharama ya antibiotiki na chanjo watakazotumia mpaka kufikia uzalishaji V. Gharama ya umeme Sio lazima uwe na pesa yote kwa pamoja ndio uanze ufugaji wa kuku chotara, bali unaweza kuanza hata kama unarobo ya pesa inayohitajika. Kikubwa uainishe vyanzo vya pesa itakayotumika kuendeleza mradi. #kuroiler #chotara