У нас вы можете посмотреть бесплатно TRUMP AJA NA MPYA, AAMURU MAREKANI KUJIONDOA WHO NA KUFUTA URAIA WA KUZALIWA или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Rais wa Marekani, Donald Trump, amesaini amri kadhaa za kiutendaji baada ya kuapishwa, ikiwemo kufuta haki ya uraia wakuzaliwa kwa watoto wa wahamiaji haramu na wenye viza za muda. Uamuzi huu umebadilisha tafsiri ya muda mrefu ya marekebisho ya 14 ya Katiba ya Marekani, ambayo yalikuwa yakitoa uraia wa kuzaliwa kwa yeyote aliyezaliwa nchini Marekani, bila kujali hali ya kisheria ya wazazi wake. Kwa mujibu wa amri hiyo mpya, watoto waliozaliwa Marekani hawatatambuliwa kama raia wa nchi hiyo iwapo wazazi wao ni wahamiaji wasio halali au wana viza za muda. Hatua hiyo itaanza kutekelezwa siku 30 kutoka sasa, na watoto watakaozaliwa nchini humo watahitajika kuwa na angalau mzazi mmoja ambaye ni raia wa Marekani au mkazi wa kudumu mwenye kadi ya kijani. Marekebisho ya 14 ya Katiba ya Marekani, yaliyopitishwa zaidi ya karne moja iliyopita, yamekuwa msingi wa uamuzi wa Mahakama ya Juu yanayowalinda watoto wa wazazi wa kigeni waliozaliwa nchini Marekani. hivyo, Trump amenda kinyume na uamuzi huo, akisisitiza kuwa sheria za sasa zimekuwa zikivutia wahamiaji haramu kuingia nchini humo. Aidha, Trump ametia saini amri nyingine inayolenga wahamiaji haramu waliopatikana na hatia za makosa makubwa ya jinai. Kwa mujibu wa amri hiyo, wahamiaji hao sasa watakabiliwa na adhabu ya kifo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kupambana na uhalifu unaodaiwa kusababishwa na wahamiaji wasio halali. Hatua hizo zimeibua mjadala mkali miongoni mwa wanaharakati wa haki za binadamu na wataalamu wa sheria, wakisema kuwa mabadiliko hayo yanakwenda kinyume na misingi ya haki za binadamu na Katiba. Baadhi ya wakosoaji wamedai kuwa sera hizi mpya zinaweza kuongeza mgawanyiko wa kijamii na kushusha hadhi ya Marekani kama nchi yenye historia ya kukaribisha wahamiaji. Katika hatua nyingine, Rais Trump amesaini amri ya Marekani katika uanachama wa Shirika la Afya Duniani (WHO). "Oooh, hii ni kubwa,” amesema Rais Trump baada ya kuletewa nyaraka za kusaini kujiondoa katika uanachama wa shirika hilo baada ya kusaini amri kadhaa nchini humo ikiwemo ya kuwataka wasiyo raia wa taifa hilo na wanaoishi Marekani bila kibali kuanza kujiondoa. Hiyo ni mara ya pili kwa Trump kuamuru Marekani ijiondoe WHo. Pia aliwahi kutaka Marekani ijiondoe kufuatia namna ambavyo ilikuwa inashughulikia mlipuko wa Ugonjwa wa Uviko-19 mwaka 2019. Hata hivyo, uamuzi huo ulitenguliwa baadae na Rais Joe Biden alipoingia madarakani. "Walikuwa (WHO) wakitutaka turejee vibaya mno kwenye shirika hilo sasa ngoja tuone itakuwaje,” amesema Trump. Kwa mujibu wa Trump uwepo wa Marekani katika Shirika hilo unaisababishia mzigo mkubwa kutokana na kuwa mchangiaji mkuu wa fedha ikilinganishwa na mataifa mengine yenye idadi kubwa ya watu akitolea mfano China.