У нас вы можете посмотреть бесплатно HISTORIA YA JENISTA MHAGAMA hadi kifo chake leo или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
#usikutv #thebesthistory #Jenista #Joakim #Mhagama #usikutv Jenista Joakim Mhagama (23 Juni 1967 - 11 Desemba 2025 alikuwa mbunge wa jimbo la Peramiho katika bunge la kitaifa nchini Tanzania[2] akitokea katika chama cha CCM. Aliwahi kuwa Waziri katika serikali ya awamu ya nne, ya tano[3] na ya sita vilevile. Elimu na kazi Jenista kwa kabila alikuwa Mngoni. Alimaliza elimu yake katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Peramiho mwaka 1986. Mwaka 1989, alipata Diploma ya Elimu kutoka Chuo cha Ualimu Korogwe. Alifanya kazi kama mwalimu kwa miaka sita kati ya 1991 na 1997. Maisha ya siasa Mhagama alianza kujihusisha na CCM mwaka 1987 na kuhudumu katika nyadhifa mbalimbali zikiwemo za tawi la vijana na wanawake wa chama hicho. Aliteuliwa kwa mara ya kwanza katika Bunge kuwa mbunge wa kiti maalum kilichotengwa kwa ajili ya wanawake mwaka wa 2000. Mwaka wa 2005, alimshinda aliyekuwa Waziri wa Fedha Simon Mbilinyi katika mchujo wa haki ya kuiwakilisha CCM katika uchaguzi ujao wa jimbo la Peramiho. Ilitokana na uchambuzi uliogundua kuwa Mhagama alikuwa mbunge wa pili kwa wingi wa michango ya mijadala na maswali kwa mawaziri katika Bunge la 2005-2010. Mhagama alikuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi katika utawala wa Rais Jakaya Kikwete kati ya Januari 2014 na Januari 2015. Katika uchaguzi mkuu wa 2015, Mhagama alishinda kiti chake cha Peramiho dhidi ya mgombea wa CHADEMA Erasmo Mwingira kwa kura 32,057 dhidi ya 11,462 Katika baraza jipya la mawaziri la Rais John Magufuli, mnamo Desemba 2015, alipandishwa cheo na kuteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Mnamo Januari 2022, alihamishwa hadi Ofisi ya Rais Utawala Bora na Huduma za Umma