У нас вы можете посмотреть бесплатно CHUO CHA KIMATAIFA CHA UVUVI KUJENGWA BAGAMOYO или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inatarajia kujenga chuo kipya Uvuvi chenye hadhi ya kimataifa kitakachokuwa chini ya Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi nchini (FETA) kampasi ya Mbegani Bagamoyo mkoani Pwani. Hayo yamebainishwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt.Bashiru Ally kakurwa alipotembelea kampasi hiyo Februari 12, 2026 ambapo ameeleza kuwa chuo hicho kitakuwa cha kisasa zaidi kwenye eneo la utoaji wa mafunzo ya uvuvi, miundombinu ya kufundishia, mifumo ya kiteknolojia, vifaa vya kufundishia na uwezo wa wakufunzi. "Nafurahi kusikia mmeunda kamati ya mazungumzo baina ya Chuo kwa niaba ya Wizara na Mamlaka ya bandari na kamati hiyo isiwe na picha ya chuo kilichojengwa wakati Mwalimu Nyerere anahangaika kujenga Taifa bali kiwe na hadhi inayofanana na kumbukizi ya baba wa Taifa" Amesema Balozi Dkt Bashiru. Mbali na ujenzi wa chuo hicho, Balozi Dkt. Bashiru amesema Serikali inatarajia kununua meli mpya ya uvuvi kwaajili ya shughuli za mafunzo. Naye Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh amesema kuwa shughuli za uvuvi nchini haziwezi kufanyika bila kuwa na mafunzo yatakayowawezesha wataalam hususan wale wa ndani kufanya shughuli hizo kwa ufanisi na uaminifu.