У нас вы можете посмотреть бесплатно USIIZIKE NDOTO YAKO (DON'T BURY YOUR DREAM) REV. DR. ELIONA KIMARO или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH : IBADA YA JUMAPILI YA KUSIFU NA KUABUDU - 05 /10/2025 UJUMBE WA LEO: USIIZIKE NDOTO YAKO (DON'T BURY YOUR DREAM) 2 Wafalme 6 : 1 - 7 Matendo 26 : 19 2 Wafalme 6 : 1 - 7 1 Kisha, wana wa manabii wakamwambia Elisha, Angalia basi, mahali tukaapo mbele yako ni padogo kwetu. 2 Basi twende mpaka Yordani, twakuomba, tutwae huko kila mtu mti mmoja, ili tujifanyie huko mahali pa kukaa. Akajibu, Haya! Nendeni. 3 Mmoja wao akasema, Uwe radhi, basi nakusihi, uende pamoja na watumishi wako. Akajibu, Nitakwenda. 4 Basi, akaenda pamoja nao. Nao walipofika Yordani, wakakata miti. 5 Lakini mmojawapo alipokuwa katika kukata boriti, chuma cha shoka kikaanguka majini; akalia, akasema, Ole wangu! Bwana wangu, kwani kiliazimiwa kile. 6 Mtu wa Mungu akasema, Kilianguka wapi? Akamwonyesha mahali. Akakata kijiti, akakitupa pale pale, chuma kikaelea. 7 Akasema, Kiokote. Basi akanyosha mkono, akakitwaa. Matendo 26 : 19 19 Kwa hiyo, Ee Mfalme Agripa, sikuyaasi yale maono ya mbinguni, HOJA ZA KIFALSAFA NA KITHEOLOJIA: 1. MAWAZO YA KUONGEZEKA NA KUPANUKA YANAENDA SAMBAMBA NA MIKOPO NA UHITAJI WA NGUVU NA USAIDIZI WA ZIADA. "KUAZIMA CHUMA CHA SHOKA" ■KUFANYA KAZI CHINI YA MTU KAMA YAKOBO NYUMBANI KWA LABANI NA YUSUFU NYUMBANI KWA POTIFA. 2. KUPOTEZA NA KUINGIA KWENYE MADENI WAKATI UKIWA NA NDOTO KUBWA YA KUONGEZEKA NA KUZALISHA. ■Reff. ADAMU NA HAWA WALIPO POTEZA WATOTO WAO WAWILI WA KIUME WAKIWA NA NDOTO KUBWA YA BARAKA YA KI-VIZAZI NA KUIJAZA DUNIA. (THE FIRST FAMILY CHALLENGE:) 3. KUPOTEZA WAKATI UKIWA UWEPONI MWA MUNGU. CHUMA CHA SHOKA KILIPOTEA NA KUZAMA MAJINI NABII ELISHA AKIWEPO NA KAZI YA UJENZI WA NYUMBA YA MUNGU UKIWEPO. ■BADALA YA KUZIKA NDOTO MWAMBIE ELISHA WAKO. NIONYESHE CHUMA CHA SHOKA KILIANGUKIA WAPI? ■UWE NA MADHABAHU YENYE MAJIBU. 4. USIYAASI YALE MAONO YA MBINGUNI... NDOTO NYINGI HUFIA KWENYE JAMII INAYOKUZUNGUKA. SOCIAL INTERACTIONS & CHALLENGES. JAMII NI ADUI NA MUUAJI WA NDOTO YAKO. ■SIPORA MKE WA MUSA NA SOCIAL CHALLENGES YA KUPIGANA NA WANAUME KILA SIKU KISIMANI MPAKA SIKU ALIPOKUTANA NA MUSA HAPO KISIMANI. Kutoka 2 : 16 - 21 16 Basi kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao wakaja wakateka maji, wakazijaza birika maji, wapate kunywesha kundi la baba yao. 17 Wachungaji wakaja wakawafukuza; lakini Musa akasimama, akawasaidia, akalinywesha kundi lao. 18 Walipofika kwa Reueli baba yao, akasema, Imekuwaje hata mkarejea mapema leo? 19 Wakasema, Mmisri mmoja alituokoa katika mikono ya wachungaji, tena zaidi ya hayo, akatutekea maji, akalinywesha kundi. 20 Akawaambia binti zake, Yuko wapi basi? Mbona mmemwacha mtu huyo? Mwiteni, ale chakula. 21 Musa akawa radhi kukaa kwake mtu yule, naye akampa Musa binti yake, Sipora. TUSIWANYIME WATOTO FURSA YA KUPATA CHANGAMOTO ZA KIJAMII NA ZIWASAIDIE KUJIJENGEA UWEZO BINAFSI WA KUJIPAMBANIA. LEO TUNA KIZAZI CHA READY MADE DUNIA HAINA HURUMA. LAZIMA KUWA NA NGOZI NGUMU: MALAIKA ALIPOTUMWA NA MUNGU KUJA DUNIANI KWA DANIELI ALIZUILIWA NJIANI SIKU 21 NA MKUU WA UAJEMI NA MALAIKA MIKAELI MPIGANAJI AKAJA KUMSAIDIA NA AKARUDI TENA KUPIGANA WAKATI ANARUDI MBINGUNI NA BAADAYE VITA IKAHAMIA KWA DANIELI. Danieli 10 : 12 - 21 12 Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako. 13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi. 14 Sasa nimekuja kukufahamisha mambo yatakayowapata watu wako katika siku za mwisho; maana maono hayo ni ya siku nyingi bado. 15 Na alipokwisha kusema nami maneno hayo, nikauelekeza uso wangu chini, nikawa bubu. 16 Na kumbe, mmoja mfano wa wanadamu akanigusa midomo yangu; ndipo nikafumbua kinywa changu, nikanena, nikamwambia yeye aliyesimama karibu nami, Ee Bwana wangu, kwa sababu ya maono haya huzuni zangu zimenipata tena; hata sikusaziwa nguvu. 17 Maana, mtumishi wa Bwana wangu huyu atawezaje kusema na Bwana wangu huyu? Kwa maana kwangu mimi, mara hazikusalia nguvu ndani yangu, wala pumzi haikusalia ndani yangu. 18 Kisha mmoja mfano wa mwanadamu akanigusa tena, akanitia nguvu. Mhubiri: Rev.Dr. Eliona Kimaro Kwa maoni na ushauri: Smu :+255655516053, +255754516053 YouTube : Rev. Dr. Eliona Kimaro TV Barua Pepe: [email protected]