У нас вы можете посмотреть бесплатно UPUNGUFU WA MAJI MWILINI: Sababu, Dalili, Matibabu, Kuzuia или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Katika video hii inazungumza kuhusu sababu, dalili, matibabu, namna ya kuzuia, matarajio baada ya matibabu ya UPUNGUFU WA MAJI MWILINI (Kupungukiwa maji) , endelea angalia mpaka mwisho kujifunza Upungufu wa maji mwilini unapokuwa mkubwa sana unaweza kutishia maisha. Ukipungukiwa maji mwilini inamaanisha kwamba seli na tishu zinakauka na kushindwa kufanya kazi. Unaweza kupungukiwa maji mwilini baada ya kupoteza maji mengi zaidi kutoka mwilini au kutokunywa maji ya kutosha. Mwili wako unaweza kupoteza maji mengi kwa: • Kutokwa jasho jingi kuliko kawaida (kwa mfano, wakati wa mazoezi) • Kukojoa sana kuliko kawaida - mtu mwenye kisukari ambaye hayuko kwenye matibabu au baada ya kutumia dawa za kutoa maji mwilini –diuretics • Homa • Kutapika na kuhara Unaweza usinywe maji ya kutosha kama: • Umepoteza hamu ya kula kwa sababu ya ugonjwa • Kichefuchefu au kama • Unawashwa au maumivu kooni na vidonda mdomoni Watoto wadogo wako kwenye hatari zaidi ya kuishiwa maji mwilini kuliko ilivyo kwa watu wazima. Hii ni kwa sababu ya uzito wao mdogo na miili yao- wanaweza kupoteza maji haraka sana kuliko ilivyo kwa watu wazima. Wazee na watu wazima wanaougua wako kwenye hatari zaidi pia. Dalili za upungufu wa maji mwilini? • Midomo mikavu • Kiasi cha mkojo kinapungua sana, mkojo unakuwa wa njano sana • Hakuna machozi • Macho yanadumbukia ndani • Utosi wa mtoto mchanga unadumbukia ndani • Uchovu , kizunguzungu, kuchanganyikiwa na hata kupoteza mpaka fahamu hali ikiwa mbaya sana Wakati gani utafute matibabu ya haraka? Ni vizuri kuonana nan a daktari kama unadhani kiasi cha maji unachompatia mwanao hakimtoshi. Pia, ongea na mtumishi wa afya: • Kama wewe au mwanao mgonjwa anashindwa kula chochote au kunywa chochote - bila kutapika au kuharisha. • Kama umekuwa ukitapika kwa zaidi ya masaa 24 kwa mtu mzima au kwa zaidi ya masaa 12 kwa mtoto • Kama kuhara kumedumu kwa zaidi ya siku 5 kwa mtu mzima au mtoto • Kama mwanao mchanga au mwanao mkubwa amenyong’onyea sana kuliko kawaida • Kama wewe au mwanao anakojoa sana kuliko kawaida, hasa kama kuna historia ya kisukari kwenye familia yako au kama unatumia madawa ya kupunguza maji mwilini Utambuzi wa upungufu wa maji mwilini Dakitari anaweza kufanya uchunguzi wa mwili na kuagiza vipimo ili kuangalia mwili wako umepoteza kiwango gani cha madini kama sodiamu, potasiamu, na bicarbonates . Atafanya pia vipimo vya damu kuangalia mifumo mingine ya mwili kama figo inafanya kazi vizuri. Anaweza pia kuagiza Vipimo vingine ili kujua sababu ya upungufu wa maji mwilini (kwa mfano, kiwango cha sukari kwenye damu ili kuangalia ugonjwa wa sukari. Uchaguzi wa matibabu wa upungufu wa maji mwilini Kunywa maji ya kutosha kunasaidia kuongeza maji mwilini na kuondoa upungufu wa kadiri wa maji mwilini. Kunywa maji kidogo kidogo - kwa kutumia kijiko au bomba la sindano kwa watoto wachanga. Kunywa kidogogo kidogo badala ya kujilazimisha kunywa maji mengi sana kwa wakati mmoja. Kunywa maji mengi sana kwa wakati mmoja kunaweza kusababisha utapike. Tumia mchanganyiko wa ORAL - ORS-Oral Rehydration Salt ili kutibu upungufu wa maji kama mtoto anaweza kunywa. Zingatia maelekezo yaliyo kwenye pakiti ya jinsi ya kuichanganya na jinsi ya kuitumia. Usitumie maji ya kawaida kumtibu mtu anayehara sana. Maji ya kawaida hayana madini na chumvichumvi za kutosha kuurejesha mwili katika hali yake. Wagonjwa wenye upungufu wa maji wa wastani au mkubwa sana wanaweza kulazwa hospitalini ili kuongezewa maji kwenye mishipa. Tiba ya aina hii inawafaa zaidi wagonjwa waliopoteza fahamu au walionyong’onyea sana. Baadae wakiweza kula na kunywa tena waanze kupewa ORS. Kesi nyingi za kuharisha na kutapika husababishwa na virusi, kwa hiyo zinapona zenyewe bila matibabu yoyote. Kuzuia upungufu wa maji mwilini Hata unapokuwa na afya njema, kunywa maji mengi kila siku. Kunywa mengi zaidi kunapokuwepo na joto au wakati unapofanya mazoezi. Kuwa mwangalifu unapowahudumia wagonjwa, hasa watoto wachanga, watoto wakubwa au wazee. Kama ukihisi kuwa mgonjwa anapata upungufu wa maji , mwone mtoa huduma za afya kabla hali haijawa mbaya zaidi. Mpatie maji mgonjwa baada tu ya kuanza kuharisha au kutapika. USISUBIRI mpaka utakapoona dalili za upungufu wa mwili. Mara zote, mshauri mtu yeyote anayeumwa anywe maji ya kutosha. Kumbuka pia mahitaji ya maji mwilini yanaongezeka wakati wa homa, kutapika au kuharisha. Njia rahisi ya kumtambua mgonjwa ambaye anakunywa maji ya kutosha ni kuangalia kiasi cha mkojo anachotoa. Emmanuel Mniko #mniko #wikielimu @wikielimu