У нас вы можете посмотреть бесплатно Mfalme Zumaridi ukweli wote hadharani , shahidi ajitokeza, aeleza ukweli wa mambo yote. или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Kesi ya Mfalme Zumaridi , ukweli hadharani shahidi ajitokeza, aeleza ukweli wa mambo yote. katika kesi inayomkabili mfalme zumaridi na wenzake 8, siku ya leo kesi imeendelewa kusomwa ambapo Christina Mwisongo 46, Shahid wa jamuhuri. ambaye ni Afisa ustawi wa jamii Halmashauri ya Jiji la mwanza.(kulinda na kutetea haki za watoto) ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua stahiki juu ya kumuokoa mtoto anapokuwa katika mazingira hatarishi na kupokea amri zote za mahakama zinazohusu madai ya kesi ya watoto zinazofika mahakamani kwa kushirikiana na jeshi la polisi Akitoa ushahidi alisema kuwa "Mnamo tarehe 22.2.2022 alifika wakili Linus Mnishi akiwa na Ally Abas Shabani Baba wa mtoto SS wakiwa wameleta Amri ya mahakama kwa Afsa ustawi wa jamii ya kumchukua mtoto SS wakiwa na nakala ya hukumu ya madai ya taraka iliyofunguliwa Mahakama ya Mwanzo mkuyuni wakitaka ofisi ya ustawi wa jamii kutekeleza Amri hiyo ya kuchukua mtoto. Hivyo mkuu wake wa kazi kumuhamru kufuatilia kesi hiyo ambaye ni AFISA ustawi wa jamii wilaya. Shahidi huyu ametambua vithibitisho ambavyo ni Amri ya mahakama pamoja na Nakala ya hukumu ya Taraka Baada ya kuipokea aliandika mwasiliano ya Wakili Linus pomoja na Baba wa mtoto SS ambavyo aliandika mwenyewe kwa kalamu ya bluu Ushahidi ulipokelewa na mahakama huku upande wa utetezi wakiupokea pia bila pingamizi Hukumu ya madai ya Taraka ilisomwa mahakamani na kubaini kuwa ilitolewa 23.09.2020 kuwa mdai aliomba Taraka na hifadhi ya mtoto SS baada ya ambapo mahakama haikutoa Taraka kwa kuwa hakukuwa na ndoa na kutoa hukumu kwa hifadhi ya mtoto SS kwa Baba yake ambaye ni mdai katika kesi hiyo. Na kutoa Amri kwa ustawi wa jamii kufuatana na Askari polisi kwenda kumchukua mtoto na kumrejesha mahakamani ili akabidhiwe kwa Baba yake mzazi ikiwa. Aliambatana na Askari kwenda Nyumbani kwa Zumaridi ilikumchukua mtoto SS. wakati wa kushuka katika la polisi katika nyumba hiyo alikuja kijana na kuwaambia subirini niwafungulie geti akaingia ndani na kufunga geti hilo bila kulifungua tena. Mkuu wa msafara huo akachukua hatua ya kugonga geti hilo ili kufunguliwa bila mafanikio Askari mmoja akwaambia kuwa kuna geti lingine upande wa pili ambalo lilikuwa wazi wakabahatika kuingia. Baada ya taarifa za uchunguzi wa kijamii kuwa mtoto SS anaishi pamoja na mama yake ambaye ni Suzanna Simoni nyumban kwa Zumaridi Askari alienda na kufungua geti alilogoma kufungua kijana huyo na kuruhusu Hari la polisi kuingia ndani Baada ya kushuka katika gari la polisi kiongozi wa msafara alijitambulisha na kuutambulisha msafara wake na kuhitaji kuonana na Zumaridi ambapo walikosa ushirikiano na kuambiwa hawajui alipo na kuwafuata waimbaji walioonekana mbele yao na kuwafuata, wakawasalimia pasina kujibiwa na kuwaamuru waache kuimba wawasikilizi ndipo wakaanza kusikilizwa wakiomba kuelekezwa alipo Zumaridi ambapo walijibiwa na mwalimu wa kwaya kuwa yeye yupo kwaajili ya kufundisha wanakwaya na yeye hakuwa msemaji pale na kuwataka warudi mapokezi Baada ya kujibiwa hivyo wakazidi kwenda mbele walikuta watu wengi wanaume kwa wanawake waliovali mashati meupe na sketi na suruali nyeusi wakiwa sebuleni wakiwa wanasali kwa kushikana mikono. #zumaridi#mwanza#mahakamani Wakasimama nakusubiri wamalize kusali, baada ya muda kidogo waliaanza kuunguruma kama Simba na kunYanyuka huku wakitembea mwendo wa ajabu hali iliyowafanya wao na msafara mzima kuanza kutoka nje watu hao wakiwa na Zumaridi wakamkamata Askari mmoja aliyetajwa kwa jina la Afande James kwa kumvuta, kumkanyaga na kumpiga mateke wakiendelea kuunguruma Wakashikwa na taharuki wakamwacha Afande James ambaye aliendelea kujiokoa akafanikiwa kutoka na wote wakatoka katika lango hilo na kushindwa kutekeleza Amri ya mahakama. Huku wakifuatwa na mashambulizi na kurushiwa vitu mbalimbali vikiwemo viti wakatoka nje ya geti na gari likiwafuata kwa nyuma wakaingia ndani ya gari la polisi ambapo Baba wa mtoto SS alimwonyesha mama wa mtoto wake akiwa miongoni wa watu hao aliokuwa wakizomea. Katika tukio Hilo Shahidi aliweza kumtambua Zumaridi na Suzanna Simoni ambao walikuwepo mahakamani hapo Baada ya hapo dereva aliwasha gari na kwenda kwa mbele kidogo na kupaki pembeni kumsikiliza Afande James aliyeumizwa na kuondoka huku Afande James akidai kwenda kufungua kesi na wao kurejea kituo cha Kati Nyamagana kutoa taarifa kuwa wameshindwa kutekeleza Amri hiyo Akimhoji Shahidi huyo , Wakili wa utetezi Wakili Mutta alimuuliza kama aliieleza mahakama kuwa aliwaambia polisi kuwa ana Amri ya mahakat? Kweli Anatakiwa kuhakikisha kunakuwa na amani katika jamii. #zumaridi#mwanza#mahakama