У нас вы можете посмотреть бесплатно Boshen anavyoiheshimisha fani ya uchoraji tattoo || ataja changamoto anazopitia 'wapo wanaonitaka ' или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Cheza sasa kupitia https://shorturl.at/jqzU6 na ushinde Mtaani wapo wenye mitazamo ya kuwa tattoo ni uhuni, na wengine wakikazia kwamba mwanamke mwenye tattoo siyo wa kuoa na kumweka ndani, huku kwa upande wa wanaume wenye michoro hiyo mara nyingi wakionekana wahuni na wababaishaji. Mitazamo yote hii juu ya watu hao imekanushwa na mchora tattoo maarufu Tanzania , Bryson Peter maarufu kama Boshen, kwa kusema kuwa tattoo ni michoro kama mingine na ni sanaa ambayo haina uhusiano wowote na uhuni kama watu wanavyodhani. Boshen ambaye alianza kazi ya uchoraji tattoo miaka kumi iliyopita, kipaji chake kilianza kuonekana tangu akiwa shule ya msingi kwa kuwachorea wanafunzi wenzake picha mbalimbali. Wakati akizungumza na gazeti hii amesema uhuni siyo muonekano, ni tabia ya mtu. Boshen amesema ili mtu aweze kuwa mchoraji mzuri wa tattoo ni lazima awe na kipaji cha kuchora, pia katika utendaji ni lazima awe na vifaa vya kisasa. Huku akitaja kuwa hiyo ndiyo sababu kubwa ya watu wengi kumfuata awapatie huduma hiyo. “Kuna watu wanatumia vifaa ambavyo siyo vya kisasa, sindano wanarudia, kuna wengine wanachemsha mimi kazi zangu huwa nafanya asilimia mia vifaa vipya, natumia natupa, kwa hiyo kama mchoraji unatakiwa uwe na uelewa wa hii kazi na uipende”. Amesema. Boshen anasema vifaa vya kuchorea tattoo ni gharama na Tanzania havipatikani hivyo wakati wa kuviagiza huchukua muda kufika, kwa upande wake inamlazimu kuwa na akiba ya kutosha kwa kuwa amekuwa akipata kazi mpya kila mara. Ametaja bei ya boksi la sindano za kuchorea tattoo ni Sh 100,000 ndani yake lina sindano 50, wino na vifaa vingine pia huviagiza nje ya nchi. Usikofe kufuatilia video kamili katika YouTube Mwananchi Digital.