У нас вы можете посмотреть бесплатно Sayansi darasa la nne _ mada ya kwanza_ kanuni za afya или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Dhana ya kanuni za afya Kuzingatia kanuni za afya ni jambo la muhimu ili kudumisha ~afya bora. Afya bora ni hali ya kuwa imara kimwili na kiakili. -Ili kuwa na afya bora ni lazima kuzingatia kanuni za afya. Miongoni mwa kanuni hizo ni (i) kula mlo kamili (ii) kufanya mazoezi ya mwili. (iii) kuzingatia usafi wa mwili na mazingira. (iv) kuzingatia alama na taarifa muhimu katika mazingira. MLO KAMILI Mlo kamili ni mlo wenye virutubisho vyote vya chakula katika uwiano sahihi. Mlo kamili huundwa na vyakula kutoka katika makundi makuu matatu. (i)vyakula vya kuupa mwili nguvu. Vyakula hivyo vina virutubisho vya kabohaidreti au wanga. (ii) vyakula vya kujenga mwili vyenye virutubisho vya protini. (iii)vyakula vya kulinda mwili vyenye virutubisho vya vitamini na madini. Mlo kamili hutupatia virutubisho vyote muhimu ambavyo mwili unahitaji kwa uwiano sahihi. Umuhimu wa mlo kamili ni 🔹kuimarisha kinga ya mwili ili kuweza kupambana na magonjwa. Kielelezo kifuatacho kinaonesha mfano wa makundi makuu ya vyakula katika mlo kamili. Kazi ya kufanya namba 2 1. Bainisha vyakula mbalimbali vinavyopatikana katika mazingira yako. 2. Ainisha vyakula hivyo katika makundi makuu sahihi. (i)Vyakula vya kuupa mwili nguvu 🔹Vyakula vya kuupa mwili nguvu ni vyenye virutubisho vya wanga au kabohaidreti pamoja na mafuta. 🔹Vyakula vyenye kabohaidreti ni kama vile mahindi, viazi, mihogo, ndizi, wali na mkate. 🔹Vyakula vyenye mafuta ni kama vile nazi, karanga, mafuta na parachichi. Vyakula hivi huuwezesha mwili kuwa na uwezo wa kufanya shughuli mbalimbali zikiwemo kucheza, kulima na kutembea.Vilevile, mafuta husaidia kuupa mwili joto. Vyakula vya kujenga mwili 🔹Vyakula vya kujenga mwili ni vyenye virutubisho vya protini. 🔹Vyakula hivyo ni kama vile samaki, maziwa, nyama, mayai, njegere na maharage. Kazi ya vyakula hivi ni kujenga mwili na kuufanya ukue vizuri. Pia, vyakula hivi hutumika kutengeneza seli mpya ili kuchukua nafasi ya seli zilizozeeka au kufa. Picha ifuatayo inaonesha vyakula vya kujenga mwili Vyakula vya kulinda mwili Vyakula vya kulinda mwili ni vyenye vitamini na madini. Kazi ya vyakula vya madini 🔹Vyakula hivi husaidia kuimarisha afya na kuwezesha mwili kujikinga na magonjwa. 🔹Pia, husaidia kujenga na kuimarisha misuli na mifupa ya mwili. Vyanzo vya vyakula vya vitamini na madini Vitamini na madini hupatikana katika mbogamboga kama vile kabichi, sukumawiki, mchicha, biringanya na karoti. 🔹Pia, hupatkana katika matunda mfano papai, chungwa, parachichi, zabibu na embe. Maji Kazi za maji 🔹Maji si sehemu ya makundi makuu ya vyakula yanayounda mlo kamili. Hatahivyo, mwili huhitaji maji ya kutosha ili uweze kufanya kazi ipasavyo. Hii ni kwa sababu yana madini mbalimbali yanayosaidia mifumo ya mwili kufanya kazi vizuri. Kwa mfano, umengenywaji wa chakula na ufyonzwaji mzuri wa virututisho kutoka kwenye vyakula. Pia, maji husaidia kuondoa takamwili na sumu mwiini. Vilevile, maji husaidia kurekebisha joto la mwili.