У нас вы можете посмотреть бесплатно AKAMATWA AKITOROSHA MADINI YA DHAHABU KILO 4.3 YENYE SAMANI YA MILIONI 562 KAHAMA или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imemkamata Mafanyabiasha wa Madini ya Dhahabu Devrat Kerai Mwenye asili ya andia ambaye ailikuwa akitaka kutorosha madini ya Dhahabu yenye jumla ya kilo 4.3 na thamani ya shilingi milioni 562 na kusababishia serikali pia kukosa mapato yake. Mfanyabiashara huyo Mwenye kumiliki Kampuni ya Nadoyo Mineral Trading Limited Dervat Kerai alikamtwa juzi katika nyunmba ya kulala wageni ya Niteshi Mji Kahama majira ya saa moja usiku na maafisa wa serikali ambao walikuwa wakifuatia nyendo zake baada ya kufanya tukio hilo. Hayo yalisemwa juzi na Waziri wa Madini wa Madini\ Anthon Mavunde wakati akiongea na Wanunuzi wa madini wa Madini ya Dhahabu katika soko kuu la Kahama na kuongeza kuongeza kuwa bado serikali inaendelea na uchunguzi ili kubaini wale wote ambao wanashirikiana nae katika suala zima la utoshaji madini. Mavunde alisema kuwa alisema kuwa serikali serikali ahiwezi kuvunmilia wale wote ambao wanajihusisha katika suala zima la utosahi madini na kuongeza kuwa ni bora wakawa wanafuata taratibu zote zilizowekwa ili waweze kufanya biasha biasahara hiyo kwa uhuru na haki bila ya kubugudhiwa Waziri Mavunde ambaye alikuwa njiani kuelekea katika ziara Mkoa wa Geita alisema kuwa wafanyabiashara ambao wamekuwa wakitorosha madini wamekuwa wakiikoseha Nchi kukosa mapato yake na kuongeza kuwa hali hiyo inafnya na mtandao mkubwa ambao kwa sasa serikali inaujua. Hata hivyo Waziri Mavunde alifurahishwa kuona katika soko la Madini ya Dhahabu katika Wilaya ya Kahama kundi kubwa linalofanya biashara hiyo kuwa ni vijana na kuhaidi Serikali kuwaunga mkono ili waweze kuwa wafanyafanyabiashara wakuwabwa katika siku za baadaye. “Ninafurahishwa na kukuta Wafanyabiashara wa madini ya Dhahabu katika Wilaya ya Kahama asilimia kubwa kuwa ni vijana ambao wamekuwa wakichangamkia uchumi wa wa madini, mmi nitakuwa pamoja na nyinnyi lengo kubwa ilikuwa ni kuhakikisha kuwa unakuwa wakubwa katika biashara hiyo”, Alisema Mavunde Waziri wa Madini. Aidha Waziri huyo wa Madini alisema Wafanyabiashara wa madini kwa sasa lazima wafutate sheria na taratibu za serikali katika kazi zao na kuongeza kuwa yule ambaye atakamatwa akitorosha madini serikali itafuta leseni zake zote katika maeneo yote ambayo nafanya kazi akianzia na kampuni hiyo ya Nadoyo Mineral trading Limited. Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mboni Mhita alisema kuwa Wilaya ya Kahama imekomaa katika utoroshaji wa Madini ya Dhahabu na kuongeza kuwa serikali kwa sasa imekuja upya na kuongeza kuwa serikali ya Tamzania ni moja, ukitorosha madini nui sawa na kuhujumu uchumi wan chi. Mhita alisema kuwa ukitorosha madini ni sawa na kuwakatisha tama wafanyabiasha wengine ambao wanafuata taratibu na sheria za nchi na kuwataka wengine waache tabia hiyo kwa serikali hitawafumbia macho ikiwa ni pamoja na kuwafikisha katika vyombo vya sheria. Nae Afisa Madini Mkazi Wilaya ya Kahama Jeremiha Hango aliiomba serikali kuhakikisha kuwa wale wote wafanyabiashara wanaokamatwa wakitorosha madini Nchini wanafutiwa leseni zao katika maeneo yote ambayo wanakuwa wakifanya biashara hiyo hapa nchini. Alisema kuwa katika Wilaya ya Kahama kuna soko moja la Madini lakini kuna vituo sita vya ununuzi na kuiomba serikali kuona njinsi ya kutatua matatizo makubwa yaliopo kwa wafanyabiashara wa madini ya mtu mmoja akifanya kosa katika sehemu moja leseni yake isimamishwe katika maeneo yote hapa nchini ambayo anamiliki. Hata Hivyo Mwenyekiti wa soko la Madini Wilaya ya Kahama Emanuely Kidenya alise ma kuwa wale wote ambao wamekuwa wakifanya makosa na wasio waminifu ni bora ndio wanaoleta changamoto kwa wafanyabiashara wa madini katika Wilaya ya Kahama. Aliendelea kusema kuwa kuwa biashara hivyo imekuwa na mnyororo mkubwa huku akisisiza kuwa wao kama wafanyabiashara wa dhahabu wapo tayari kutoa ushirikiano serikali ili kuwabaini wale wafanyabiashara wasio waaminifu ambao wamekuwa wakitorosha madini hayo ya dhahabu. KITUO KINACHO JIHUSISHA NA HABARI MBALIMBALI ZA KIJAMII NA KUELIMISHA UMMA KUHUSU MATUKIO YANAYO JIRI KILA WAKATI HAKIKISHA UNA SUBSCRIBE CHANEL YETU USIPITWE NA TUKIO LOLOTE HAPA NCHINI ( Email: [email protected](+255752268249 / +255785537878)