У нас вы можете посмотреть бесплатно NINI MAANA YA UPENDO? или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
NINI MAANA YA UPENDO? Upendo ni hali ya moyo isiyo na uchungu, kinyongo, au chuki dhidi ya wale wanaotuumiza au kututendea mabaya. Ni hali ya kumwachilia mtu huru moyoni mwako, hata kama amekuudhi au kukutendea uovu. Katika maisha, mara nyingi tunakutana na watu wanaotuumiza kwa maneno, matendo, au hata kwa hila. Maadui ni wengi kuliko marafiki wa kweli. Wakati mwingine, unaweza kudhani unapendwa kumbe ni kinyume chake. Lakini upendo wa kweli haupimwi kwa jinsi unavyotendewa, bali kwa jinsi unavyoweza kuonyesha neema hata kwa wale wasiostahili. Tatizo kubwa linalotuzuia kupenda ni kinyongo. Wengi tunashindwa kumpenda mtu aliyekosea kwa sababu bado tunabeba maumivu ya uovu wake. Hata hivyo, Biblia inatufundisha kupenda maadui zetu, si kwa sababu wanastahili, bali kwa sababu upendo wa Mungu ndani yetu unatusukuma kufanya hivyo. Upendo wa kweli si hisia za muda mfupi, bali ni uamuzi wa kudhihirisha wema hata kwa wale waliotuumiza. Kupenda adui ni jambo gumu kwa nguvu za kibinadamu, lakini kwa msaada wa Mungu, tunaweza kushinda chuki kwa upendo. Bila upendo, hatuwezi kuponya mioyo yetu wala kujenga mahusiano yenye amani. Upendo ndiyo njia pekee inayoshinda giza la chuki na visasi. Mathayo 5:43-45 “Mmesikia kwamba imenenwa, ‘Mpende jirani yako, umchukie adui yako.’ Lakini mimi nawaambia, wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, naye huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.” Warumi 12:17-21 “Msilipize mabaya kwa mabaya. Angalieni mtende yaliyo mema machoni pa watu wote. Ikiwa inawezekana, kwa upande wenu, mkae kwa amani na watu wote. Wapenzi, msijilipizie kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, ‘Kisasi ni changu, mimi nitalipa, asema Bwana.’ Lakini, ‘Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Kwa maana kwa kufanya hivyo utamwekea makaa ya moto kichwani pake.’ Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.” Askofu Subira Mitimingi #WCC