У нас вы можете посмотреть бесплатно Je ni Uzito kiasi gani Mjamzito anatakiwa kuongezeka kutoka mwanzo wa Ujauzito mpaka kujifungua??? или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Uchunguzi wa hivi karibuni uligundua kuwa karibu theluthi moja (32%) ya wanawake walipata kiwango kilichopendekezwa cha uzito wakati wa ujauzito na wanawake wengi walipata uzito nje ya mapendekezo (21% kidogo sana, 48% zaidi). Kwa kawaida Uzito wa Mama Mjamzito unatakiwa kuongezeka kuanzia wastani wa kilo 11 mpaka kilo 12.7 kuanzia mwanzoni mwa Ujauzito mpaka kujifungua. Yani Miezi mitatu ya mwanzo Mjamzito anaweza kuongezeka kilo 1 hii ni kutokana na changamoto mbalimbali mwanzoni mwa Ujauzito, huweza kuongezeka kilo 5 na pia kuongezeka kilo 5 miezi mitatu ya mwisho ya Ujauzito hivyo basi kuanzia miezi minne mpaka miezi tisa Mjamzito huongezeka kwa wastani wa kilo 1 kwa kila mwezi. Ili kuweza kujua ongezeko la Uzito wakati wa Ujauzito ni lazima kuweza kujua uwiano wa Uzito na urefu wako ambapo kitalamu huitwa Body Mass Index (BMI) na kizio chake huwa ni Kg/M² Kulingana na Uwiano wa Uzito na Urefu wa Mama husika kuna aina nne(4) za makundi ya watu. Ambazo ni:- 1. Akina Mama wenye utapia mlo ambao BMI yao huwa chini ya 18.5kg/M². Endapo upo katika kundi hili unatakiwa kuongezeka Uzito kati ya kilo 12.7 mpaka kilo 18.2 tokea ulipo pata Ujauzito mpaka kujifungua. 2. Akina Mama wenye Uzito wa kawaida ambao BMI yao huwa kati ya 18.5kg/M² mpaka 24.9kg/M². Endapo upo katika kundi hili unatakiwa kuongezeka Uzito kati ya kilo 11.4 mpaka kilo 15.9 tokea ulipo pata Ujauzito mpaka kujifungua. 3. Akina Mama wenye Uzito mkubwa kupindukia ambao BMI yao huwa kati ya 25kg/M² mpaka 29.9kg/M². Endapo upo katika kundi hili unatakiwa kuongezeka Uzito kati ya kilo 6.8 mpaka kilo 11.4 tokea ulipo pata Ujauzito mpaka kujifungua. 4. Akina Mama wenye kiriba tumbo ambao BMI yao huwa kuanzia 30kg/M² au zaidi. Endapo upo katika kundi hili unatakiwa kuongezeka Uzito kati ya kilo 5 mpaka kilo 9.1 tokea ulipo pata Ujauzito mpaka kujifungua. #MamaAfya #Uzito #DrMwanyika