У нас вы можете посмотреть бесплатно KANISA LISINGEKUWEPO HAPA IFINGA TUNGEKUFA WENGI или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
MTAZAME Mwenyekiti wa Kijiji cha Ifinga kilichopo Kata ta Matumbi Halmashauri ya Madaba wilaya ya Songea mkoani Ruvuma Gunturam Kifaru ambaye amekiri kuwa bila mchango wa kanisa katoliki kijiji hicho kingekuwa na changamoto nyingi. "Kanisa katoliki katika kijiji hiki linatoa karibu huduma zote muhimu za kijamii,ikiwemo zahanati ya misheni ndiyo inahudumia karibu watu 3000 waliopo katika kijiji hiki kwa ujumla bila kanisa wananchi wengi wangepoteza maisha kwa kukosa huduma ya afya'',anasisitiza Kifaru. Anasema padre wa parokia ya Ifinga amekuwa msaada mkubwa kuwabeba wagonjwa wanaozidiwa kuwapeleka Madaba umbali wa takribani kilometa 60 na kwamba ubovu wa barabara umechangia barabara hiyo kukosa vyombo vya usafiri ambapo gharama ya usafiri umbali wa kilometa 48 inafikia shilingi 70,000. Hata hivyo kanisa katoliki la Mtakatifu Galus Parokia ya Ifinga Jimbo Kuu katoliki la Songea lilijengwa na wamisionari wa kijerumani mwaka 1932 hivi sasa lina miaka zaidi ya 90. Kanisa hili kongwe nchini linahitaji ukarabati kwa sababu hivi sasa baadhi ya kuta zake zimeweka nyufa pia linavuja hivyo linahitaji ukarabati mkubwa ili kuliokoa lisianguke. Paroko wa Parokia ya Ifinga Padre John Otete anawaalika watu wote wanauguswa kusaidiana na waumini wa Ifinga kuchangia ukarabati wa kanisa hili. Paroko anawaalika watu wote waliopo ndani na nje ya nchi kuchangia ukarabati wa kanisa hili iwe kwa fedha taslimu au vifaa. Makadirio ya ukarabati ni fedha za kitanzania shilingi milioni 68.Unaweza kuchangia kupitia akaunti ya Benki au Simu kama ifuatavyo: 1.JINA LA AKAUNTI:PAROKIA YA MTAKATIFU GALUS IFINGA JINA LA BENKI:NMB TAWI LA SONGEA NAMBA YA AKAUNTI:61810035266 2.MWENYEKITI WA KAMATI UCHUMI NA UJENZI PAROKIA YA IFINGA MR.KINEMO KIHOMANO MPESA 0754334934 3.MHASIBU MR.GEBHARD NYONI MPESA 0754023115 4.PAROKO WA PAROKIA YA IFINGA PADRE JOHN OTETE MPESA 0756313380 KUTOA NI MOYO,CHANGIA KAZI YA MUNGU,WOTE MNAKARIBISHWA.