У нас вы можете посмотреть бесплатно RC JAMES: WAHITIMU WAEPUKE KUKIMBILIA DAR, WATUMIE FURSA ZILIZOPO IRINGA или скачать в максимальном доступном качестве, видео которое было загружено на ютуб. Для загрузки выберите вариант из формы ниже:
Если кнопки скачивания не
загрузились
НАЖМИТЕ ЗДЕСЬ или обновите страницу
Если возникают проблемы со скачиванием видео, пожалуйста напишите в поддержку по адресу внизу
страницы.
Спасибо за использование сервиса ClipSaver.ru
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, amewataka wazazi na wahitimu wa vyuo vya kati na ufundi kuachana na mtazamo wa kuelekeza maisha yao jijini Dar es Salaam, na badala yake wachangamkie fursa lukuki zilizopo katika sekta za kilimo, ufugaji na utalii ndani ya mkoa huo. Akizungumza wakati wa mahafali ya vyuo mbalimbali vya ufundi mkoani Iringa, RC James alisema vijana wengi wamekuwa na mazoea ya kukimbilia mijini mara baada ya kuhitimu, wakiamini ndiko mafanikio yalipo, hali ambayo kwa kiasi kikubwa inawadumaza kimaendeleo. "Iringa ni mkoa wenye vivutio vingi vya utalii kama Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, pamoja na ardhi yenye rutuba kwa ajili ya kilimo cha kisasa na ufugaji. Vijana wakitumia fursa hizi kwa ubunifu na bidii, wanaweza kufikia mafanikio makubwa bila kuhamia mijini," alisema. Aidha, aliwataka vijana kuanzisha vikundi vya uzalishaji, kutafuta mitaji, na kutumia rasilimali walizonazo kwa manufaa yao na jamii kwa ujumla. Alisisitiza kuwa wageni wanaotembelea Iringa hutegemea huduma za wenyeji kama chakula, burudani na utamaduni, ambavyo vyote ni fursa za kiuchumi. Katika hatua nyingine, RC James ametoa wito kwa vyuo vya kati na ufundi stadi mkoani humo kuweka mkazo katika kutoa elimu ya vitendo, itakayowawezesha wahitimu kujiajiri mara baada ya masomo. Alivitaka vyuo hivyo kuandaa programu maalum zinazowawezesha vijana kuwa wapishi wa watalii, waongozaji wa watalii wa ndani na nje ya nchi, na pia kukuza sanaa za asili za Wahehe kama njia ya kuongeza thamani ya utalii wa kiutamaduni. Mkurugenzi wa Chuo cha Turnbull, Daudi Kingalata, alitumia fursa hiyo kueleza kuwa chuo chake kilichoanzishwa mwaka 2017, kinajikita katika kutoa mafunzo ya ususi, urembo, ushonaji na kozi nyingine mbalimbali. Hata hivyo, aliomba msaada wa Serikali ili kuanzisha kituo cha ubunifu kwa ajili ya vijana wenye vipaji pamoja na kusaidiwa vifaa vya kisasa vya mafunzo kama vile majiko ya kisasa, mashine za uchapaji, vifaa vya michezo, na uboreshaji wa miundombinu ya mabweni ya wasichana. Akijibu hoja hizo, RC James aliahidi kutembelea chuo hicho ili kujionea changamoto na kuangalia namna ya kukisaidia. Aliagiza uongozi wa chuo kuwasilisha maombi rasmi kwa wakurugenzi wa halmashauri ili kupata eneo la kujenga chuo kipya.